
Asilimia
55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.
Mambo
haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha
upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).
1.
Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za
mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen
Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa
ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa
kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.
2.
Lehemu (Cholesterol).

3.
Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa
kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo
yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.
Pia,
Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza
ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia
na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna
hiyo.
Tatizo
hili pamoja na mengine mengi yanayosababishwa na ugonjwa wa kisukari huweza
kuzuiwa au kupunguzwa kwa kuzingatia masharti ya kitabibu. Katika kliniki za
kisukari wagonjwa huelekezwa namna ya kudhibiti sukari ili isizidi kiasi cha
kuleta madhara makubwa kama haya.
Asante.
Dr.Chris Cyrilo.
0 comments:
Post a Comment