Fifa Yamteua Mwanamke Wa Kwanza Kushika Wadhifa Wa Katibu Mkuu


Kwa mara ya kwanza shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA imemteua mwanamama Fatma Samba Diouf Samoura msenegali kuwa katibu mkuu wake.Bi huyu atakuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo tangu shirikisho hilo kuanzishwa.Bi Fatma anachukua nafasi ya Jerome Valcke ambae amefungiwa kushiriki masuala ya mpira kwa miaka 12.

Fatma mwenye umri wa miaka 54 amefanya kazi umoja wa mataifa kwa miaka 21 na ataanza kazi katika shirikisho la mpira wa miguu duniani mwezi June.Akinukuliwa Rais wa FIFA bwana Gianni Infantino amesema “Ni muhimu FIFA kuchukua mtazamo mpya katika juhudi za kuendelea kuijenga upya taasisi hii”.

“Amedhihirisha pasi shaka uwezo wake wa kuongoza na kujenga timu imara ya kazi na kuboresha taasisi hii katika utendaji wake.Kwa upande wa FIFA anaelewa vizuri kuwa inahitaji uwazi na uwajibikaji ambao ndio moyo wa Taasisi yoyote inayofanikiwa” alimalizia.

Hongera bi Fatma.

 
Share on Google+

About TANZANIA INVESTEMENT ADVENTURERS

We are an Investment Club geared to use social networks as means of sharing informations, knowledge, wisdom but more importantly reducing the cost of marketing your products by reaching so many potential customers with the lowest cost ever.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment